Suge Knight anamshtaki mwanamuzki
mwenza wa R& B Chris Brown mahakamani pamoja na mmiliki wa kilabu
moja ya usiku nchini Marekani kufuatia ufyatulianaji wa risasi uliotokea
katika kilabu hiyo mwaka 2014.
Mwanamuziki huyo wa zamani alipigwa risasi mara saba katika hafla ya Chris Brown.
Kesi
hiyo iliowasilishwa katika mahakama ya Los Angeles inamshtaki Chris
Brown na kilabu ya West Hollywood Ckub 1 Oak kwa kushindwa kuweka
usalama wa kutosha na kumruhusu mtu mmoja aliyejihami kuingia katika
kilabu hiyo.
Suge Knight alipigwa risasi tumboni,kifuani na mkono wa kushoto.
Kwa sasa Suge Knight anakabiliwa na kesi ya mauaji baada ya kumgonga mtu na kutoroka.
Inadaiwa kile kilichotokea katika kisa hicho ndio sababu ya yeye kufanya vitendo kama hivyo.
Alishtakiwa kwa kuwakanyaga watu wawili na kumuua mmoja huku mwengine akijeruhiwa vibaya.
Wakili wake anasema kuwa alikuwa akijaribu kuwatoroka washambuliaji .
0 comments:
Post a Comment