Mojawapo wa mwanamuziki mashuhuri mkongomani Koffi
Olomide,amejipata matatani baada ya kunaswa kwenye kamera akimpiga teke
mwanamke, anayesadikiwa kuwa mmoja wa wachezaji ngoma wake.
Tukio
hilo lilirekodiwa katika uwanja wa ndege wa Jomo Kenyatta ambako
alikuwa amewasili kwa tamasha lilopangwa kufanyika nchini Kenya.
Wengi wa Wakenya wamekashifu vikali kitendo hicho huku maoni katika
mitandao ya kijamii yakitoa wito watu kutohudhuria tamasha hilo na
badala yake wakitaka akamatwe.
Wengine kupitia kitambulisha mada #KickKoffiOlomideBackToCongo kwenye Twitter wanapendekeza afurushwe kutoka Kenya.
Kwa upande wake Koffi Olomide, kwenye ujumbe katika ukurasa wake wa Facebook, amesema tukio hilo lilieleweka vibaya.
Amesema
alikuwa anajaribu kumtetea mwanamke huyo kwani mmoja wa maafisa wa
kike katika uwanja huo wa ndege alikuwa akiwasumbua wasichana hao
wachezaji ngoma aliokuwa wakiandamana naye.
Katika video hiyo msichana huyo mchezaji anaonekana kukubaliana naye.
0 comments:
Post a Comment