Klabu ya Manchester United
inam'mezea mate Paul Pogba lakini hakuna mpango wowote wa kuonyesha kuna
mazungumzo ya kumsajili mchezaji huyo yameanza.
Uvumi umekuwepo
kuhusu uhamisho wa mchezaji huo wa pauni milioni 100 unaotarajiwa
kuvunja rekodi ya dunia,lakini BBC Sport imeambiwa kuwa hakuna
mazungumzo yoyote yalioanza kati ya Manchester United na Juventus.
Cha mno ni kwamba Pogba kwa sasa anaichezea timu ya Ufaransa na
hangependa kuathiri matayarisho yake ya fainali ya Euro siku ya Jumapili
dhidi ya Ureno.
Habari toka BBC Sport.
0 comments:
Post a Comment