Katika hali ya kushangaza star wa Hip Hop Bongo, Ibrahim ‘Roma’ Mussa’, ameondoka katika Interview aliyokuwa akifanyiwa katika kipindi cha Campus Vibe jana usiku baada ya kuulizwa swali kama anaweza kufanya ‘colabo’ na msanii mwenzie Shilole.
Roma aliulizwa swali hilo na Watangazaji wa Kipindi hicho, ambapo alijibu kwa kifupi kwamba hawezi kufanya ‘colabo’ na Shilole huku akiondoka studio kwa ‘Ghadhabu’.Katika hatua nyingine msanii huyo ameweka wazi kuwa kwa miaka 8 aliyofanya kazi na Tongwe Records yeye tayari ni Mwanafamilia wa studio hiyo.
0 comments:
Post a Comment