Watu 19 wameripotiwa kuuwawa nchini
Japan baada ya mtu mmoja kuwashambulia kwa kisu katika kituo kimoja cha
walemavu, kilichoko katika mji wa Sagamihara, magharibi mwa mji mkuu
Tokyo. Zaidi ya watu 20 wamejeruhiwa.
Ripoti nchini Japan zinasema
kuwa mtu mmoja ambaye alikuwa akifanya kazi katika kituo hicho,
alijipeleka hadi kituo cha polisi na kukiri kuwa ndiye aliyetekeleza
mauwaji hayo ya kutisha.
0 comments:
Post a Comment