Mwelekezi na mwigizaji mashuhuri wa
filamu Jackie Chan atapokea tuzo ya staha ya Oscar kwa mchango wake
mkubwa katika tasnia ya filamu.
Rais wa jopo hilo Cheryl Boone Isaacs amewataja wanne hao kama "waasisi halisi na stadi katika kazi waliyoifanya".
Chan, 62, alikuwa mwigizaji nyota katika filamu nyingi za kung-fu zilizoandaliwa katika nchi yake ya kuzaliwa, Hong Kong.
Alivuma kimataifa kwa filamu kama vile Rumble in the Bronx, Rush Hour na filamu ya vibonzo ya Kung Fu Panda.
0 comments:
Post a Comment