WAZIRI Mkuu
wa zamani, Edward Lowassa, amefunguka tena kuhusiana na utawala wa
serikali ya awamu ya tano huku akisema hakuna mtu anayemtakia mabaya
Rais John Magufuli katika kutimiza majukumu yake.
Aidha, Lowassa aliyechuana vikali na
Rais Magufuli katika uchaguzi mkuu uliofanyika Oktoba 25 wakati
alipogombea urais kwa tiketi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo
(Chadema) huku akiwakilisha pia muungano wa vyama washirika vinavyounda
Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) vya NCCR-Mageuzi, NLD na Chama cha
Wananchi (CUF), alisema kila mtu anamtakia mema Rais Magufuli ili
atekeleze vyema haki na demokrasia nchini.
Lowassa aliyasema hayo juzi usiku
wakati akihojiwa Jijini Nairobi, Kenya na Shirika la Utangazaji la
Uingereza (BBC), kuhusiana na hali ya kisiasa nchini.
Kabla ya juzi, Lowassa alishazungumza
mara kadhaa pia kuhusiana na mtazamo wake juu ya hatua mbalimbali za
Serikali ya awamu ya tano chini ya Rais Magufuli.
0 comments:
Post a Comment