Shirika la kutetea waandishi wa
habari, limelalamika juu ya kukamatwa kwa waandishi wa habari wawili wa
Jamhuri ya Demokrasi ya Congo.
Kamati ya kulinda waandishi wa
habari, CPJ, imesema wanaume hao wawili walikamatwa zaidi ya juma moja
lililopita, lakini hawakushtakiwa.
Hapo awali, waliripoti juu ya
malalamiko dhidi ya wanajeshi, kwa kuwabughudhi raia, katika mji wa
Mahagi, kaskazini mashariki mwa nchi.
CPJ inasema, waandishi wa
habari wameonewa mara kadha katika miezi ya karibuni, pamoja na
kushambuliwa, kukamatwa kiholela na mitandao kufungwa.
Uchaguzi wa rais unatarajiwa kufanywa mwaka huu katika Jamhuri ya Demokrasi ya Congo.
0 comments:
Post a Comment