Shirikisho la soka Ulimwenguni (FIFA) limetoa Ratiba ya Kombe la Dunia
kwa Klabu ambalo litadhaminiwa na Alibaba E-Auto na kufanyika huko Japan
kati ya Desemba 8 na 18.Mashindano haya yatashindaniwa na Klabu 6
Mabingwa wa Mabara pamoja na Mwakilishi kutoka Nchi Mwenyeji Japan.
Rais wa (FIFA)
Mechi za Mashindano haya zitachezwa huko Suita City Football Stadium
Mjini Osaka na International Stadium Yokohama, Mjini Yokohama ambako pia
ndipo itachezwa Fainali .
Hadi sasa Klabu 3 zimeshathibitika
kucheza michuano hiyo ambazo ni Real Madrid, Mabingwa wa Ulaya,
waliotwaa Ubingwa wao Mwezi Mei, na Timu nyingine ni Club America ya
Mexico na Auckland City FC ya Mexico Bara la Oceanic ambazo zilitwaa
Ubingwa wao Mwezi Aprili.
0 comments:
Post a Comment