TANGOZO

TANGOZO
Latest News
Friday, July 29, 2016

HILLARY CLINTON ASEMA TRUMP HAWEZI KUTATUA MATATIZO MAREKANI


Hillary Clinton amekubali rasmi kuwa mgombezi wa Urais wa Marekani kupitia chama cha Democratic, huku akisema wakati wa kupambana na mpinzani wake sasa umeanza rasmi.

Alitoa wito kwa wanachama wote wa Democratic kuungana naye huku akimkebehi mpinzani wake wa chama cha Republican, Donald Trump, katika madai yake kuwa ni yeye pekee anayeweza kuyasuluhisha matatizo ya Marekani.

Alisema kuwa Wamarekani hufanya kazi kwa pamoja kyatatua yote yanayonufaisha taifa.
  • Kiongozi wa Democratic nchini Marekani kujiuzulu
  • Bill Clinton: "Rafiki yangu" Hillary anafaa kuwa rais
Awali, bintiye Chelsea Clinton alikuwa ametoa hotuba na kumsifu sana mamake. Alisema ni mwanamke ambaye huwa hasahau anawapigania akina nani.

"Watu huniuliza kila wakati, huwa anawezaje kufanya haya? ... ni kwa sababu huwa hawasahau watu anaowatetea," amesema.

"Najua kwa moyo wangu wote kwamba mamangu atatufanya tujionee fahari."

 

  • Blogger Comments
  • Facebook Comments

0 comments:

Post a Comment

Item Reviewed: HILLARY CLINTON ASEMA TRUMP HAWEZI KUTATUA MATATIZO MAREKANI Rating: 5 Reviewed By: SIMAMA BUKOBA