Ujumbe wa California unapiga kura zao kwa ajili ya uteuzi wa mgombea kiti cha rais wa chama cha Demokratik mjini Philadelphia , Tuesday, July 26, 2016.
Ukurasa mpya wa kihistoria umeandikwa Marekani Jumane jioni, pale
wajumbe wa cha Demokratik wanaokutana huko Philadelphia, kumchagua
Hillary Rodham Clinton kua mwanamke wa kwanza kugombania kiti cha rais
kwa niaba ya chama kikuu cha kisiasa.
Uteuzi huo umefanyika baada ya wajumbe wa majimbo yote 50 kushiriki
katika upigaji kura kwa sauti Jumanne jioni, na kura 15 za ujumbe wa
Dakota Kusini zilimhakikishia kupata zaidi ya kura 2 383 zinazohitajika
ili kuweza kuteuliwa rasmi.
Waziri huyo wa zamani wa mambo ya nchi za nje anakua mgombea
rasmi wa kiti cha rais pamoja na mgombea mwenza wake Tim Kaine, baada ya
mapambano makali na Seneta Bernie Sanders, aliyetangaza rasmi hoja ya
wajumbe kumkubali kua mgombea wa chama hicho.
Hivi sasa Clinton atanaza mapambano makali dhidi ya mgombea kiti wa
chama cha republikan Donald Trump kwa ajili ya uchaguzi mkuu wa Novemba
8, 2016. Wajumbe walianza kuimba "Hillary, Hillary." baada ya matokeo
rasmi kutangazwa.
0 comments:
Post a Comment