Mtu anayedaiwa kumzaba kofi msanii Justin Timberlake katika mchuano wa gofu katika Ziwa Tahoe huko Nevada amekamatwa.
Katika
kanda ya video iliopatikana na mtandao wa TMZ,Justin anaonekana kupita
katikati ya watu kabla ya mkono wa mtu kuonekana ukimgusa upande mmoja
wa uso wake.
Justin aligeuka na kumuuliza, ndugu mbona ufanye kitendo kama hicho?
Walinzi wake walimvuta msanii huyo mwenye umri wa miaka 35 lakini baadaye akaonekana akizungumza na mshukiwa huyo.
0 comments:
Post a Comment