TANGOZO

TANGOZO
Latest News
Thursday, July 28, 2016

JITOKEZENI KUSAIDIA MAKAZI YA WAZEE NA WATU WENYE ULEMAVU NCHINI



Katibu Mkuu Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Bi. Sihaba Nkinga akisalimiana na wazee alipotembelea Makazi ya kulea wazee ya Kolandoto leo Mkoani Shinyanga.


 Afisa Mfawidhi wa Makazi ya Kulea Wazee ya Kolandoto Bi.Sophia Kang’ombe akimkabidhi taarifa ya kituo hicho Katibu Mkuu Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Bi. Sihaba Nkinga wazee alipotembelea Mkazi hayo leo Mkoani Shinyanga.

 Afisa Mfawidhi wa Makazi ya Kulea Wazee ya Kolandoto Bi.Sophia Kang’ombe akimuleza Katibu Mkuu Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Bi. Sihaba Nkinga (kulia) changamoto za Makazi hayo na kumuomba kusaidia kusimamia utatuliwaji wa matatizo hayo ikiwemo ujenzi wa majengo kwa ajili ya malazi ya wazee hao, Katikati ni Afisa Maendeleo ya Jamii kutoka Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Bi. Amina.

Katibu Mkuu Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Bi. Sihaba Nkinga akiongea na Wazee wanaoishi katika Makazi ya Kulea Wazee ya Kolandoto leo Mkoani Shinyanga na kuwahakikishia serikali kuendelea kuwasaidia kutatua changamoto zinazowakabili ili kuwawezesha kuishi katika mazingira rafiki. Katikati ni Afisa Maendeleo ya Jamii kutoka Wizara hiyo Bi. Amina… na kushoto ni Afisa Mfawidhi wa Makazi ya Kulea Wazee ya Kolandoto Bi.Sophia Kang’ombe

Afisa Mfawidhi wa Makazi ya Kulea Wazee ya Kolandoto Bi.Sophia Kang’ombe akimuonesha Katibu Mkuu Wizara ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Bi. Sihaba Nkinga sehemu ya nyumba zinazohitaji ujenzi kwa ajili ya Makazi ya Wazee hao. Wakati wa Ziara ya Kutembelea Makazi ya Wazee na kuona hali halisi ya makazi hao.
  • Blogger Comments
  • Facebook Comments

0 comments:

Post a Comment

Item Reviewed: JITOKEZENI KUSAIDIA MAKAZI YA WAZEE NA WATU WENYE ULEMAVU NCHINI Rating: 5 Reviewed By: SIMAMA BUKOBA