Kiongozi wa upinzani nchini Gambia Ousainou Darboe ameuhukumiwa kufungwa jela miaka mitatu.
Maandamano hayo yaliongozwa na Bw Darboe.
Kiongozi huyo wa upinzani alikuwa akishiriki maandamano hayo kulalamikia taarifa za kuuawa kwa mmoja wa viongozi wa chama chake, Solo Sandeng, akiwa kizuizini.
Maandamano huwa nadra sana nchini Gambia, ambayo imetawaliwa na Rais Yahya Jammeh tangu achukue madaraka kupitia mapinduzi ya kijeshi 1994.
Uchaguzi mkuu unatarajiwa kufanyika Desemba, lakini viongozi wa upinzani wanasema hautakuwa huru na wa haki.
0 comments:
Post a Comment