Bodi ya Utalii Tanzania imetoa
taarifa kufafanua kuhusu Mlima Kilimanjaro baada ya shirika moja la
habari la Marekani kudaiwa kuchapisha taarifa iliyoonekana kuashiria
mlima huo unapatikana Kenya.
Shirika hilo lilikuwa likiripoti kuhusu kifo cha Guguleth Zulu, raia wa Afrika Kusini, aliyefariki akikwea Mlima Kilimanjaro.
“Tungependa kusahihisha habari za kupotosha zilizochapishwa na
Miami Herald, kwamba Mlima Kilimanjaro unapatikana Tanzania na si
Kenya,” taarifa iliyotiwa saini na meneja mkurugenzi wa Bodi ya Utalii
ilisema.
Bodi hiyo inasema imeliandikia barua gazeti hilo na kulitaka lichapishe sahihisho.
0 comments:
Post a Comment