TANGOZO

TANGOZO
Latest News
Wednesday, July 20, 2016

MMOJA KATI YA WATOTO WA TATU (3) TANZANIA WANA TUMIKISHA

Ripoti mpya kuhusu utumikishaji watoto nchini Tanzania iliyozinduliwa hii leo inaonyesha asilimia 28 ya watoto wote wa nchi hiyo wanatumikishwa katika kazi ngumu na za hatari.

Kwa mujibu wa ripoti hiyo watoto hao wamekuwa wakitumikishwa katika maeneo hatarishi kama vile kwenye migodi ya madini, kilimo, misitu na uvuvi.

Hata hivyo ripoti hiyo inaonyesha kupungua kidogo kwa tatizo hilo ikilinganishwa na miaka kumi iliyopita ambapo watoto waliokuwa wakitumikishwa nchini humo walikuwa ni asilimia 30 ya watoto wote.

Takwimu zilizotolewa leo na ofisi ya taifa ya takwimu kwa kiasi fulani zinaonyesha matumaini kwa watoto ambao ni taifa la kesho huku lengo kubwa kwa nchi hiyo likiwa ni kutimiza azma ya malengo endelevu ya maendeleo ya dunia ya kuondoa kabisa tatizo hili ifikapo mwaka 2030.

Mkurugenzi mkuu ofisi ya taifa ya Takwimu nchini Tanzania Dkt Albina Chuwa,amesema kama ilivyo kwa tafiti zilizopita, lengo kubwa ni kupata viashiria mbalimbali vinavyoonyesha hali halisi ya utumikishwaji watoto nchini humo.

Kwa mujibu wa ripoti hiyo iliyotolewa hii leo utumikishwaji wa watoto nchini Tanzania umepungua kwa asilimia 2.8 ikionyesha mafanikio tokea takwimu za mwaka 2006.

Mojawapo ya njia zinazotumiwa na serikali ya Tanzania kuondoa utumikishwaji wa watoto ni ni uanzishwaji wa elimu bure.
  • Blogger Comments
  • Facebook Comments

0 comments:

Post a Comment

Item Reviewed: MMOJA KATI YA WATOTO WA TATU (3) TANZANIA WANA TUMIKISHA Rating: 5 Reviewed By: SIMAMA BUKOBA