TANGOZO

TANGOZO
Latest News
Monday, July 25, 2016

WHO YATOA MAFUNZO KWA WATAALAMU WA AFYA KUTOKA NCHI 14 ZA AFRICA JIJINI DAR ES SALAAM

Mtaalam na Mkufunzi wa masuala ya Afya kutoka Makao Makuu ya Shirika la Afya Duniani (WHO) Geneva,Switzarland Olau Poppe akitoa mafunzo kwa Timu ya wataalam wa Afya kutoka nchi zipatazo 14 za Bara la Afrika kuhusu mfumo wa taarifa unaotumika kutambua sababu za kifo cha mgonjwa kuwajengea uwezo watalaam hao uelewa wa ujazaji wa taarifa sahihi juu ya sababu ya kifo cha mgonjwa kwenye cheti cha kifo (Death Certificate) ili wakatoe mafunzo kwa wataalam wengine kwenye nchi zao. Mafunzo hayo ya Siku mbili yanafanyika jijini Dar es salaam.
Mtaalam na Mkufunzi wa masuala ya Afya kutoka Makao Makuu ya Shirika la Afya Duniani (WHO) Geneva, Olau Poppe akifuatilia majadiliano ya washiriki wa mafunzo ya siku 2 ya wataalam wa Afya kutoka nchi zipatazo 14 za Bara la Afrika kuhusu mfumo unaotumika kutambua  sababu ya kifo cha mgonjwa utakaowasaidia watalaam hao kujaza taarifa sahihi kwenye cheti cha kifo.

Baadhi ya Washiriki wa mafunzo kwa Timu ya wataalam wa Afya kutoka Tanzania, Zambia na Cameroon wakifuatilia miongozo mbalimbali iliyokuwa inatolewa na watalaam kutoka Makao Makuu ya Shirika la Afya Duniani (WHO) wakati wa Mafunzo kuhusu mfumo wa taarifa unaotumika kutambua sababu za kifo cha mgonjwa kuwawezesha watalaam hao kujaza taarifa sahihi juu ya sababu ya kifo cha mgonjwa leo jijini Dar es salaam.




  • Blogger Comments
  • Facebook Comments

0 comments:

Post a Comment

Item Reviewed: WHO YATOA MAFUNZO KWA WATAALAMU WA AFYA KUTOKA NCHI 14 ZA AFRICA JIJINI DAR ES SALAAM Rating: 5 Reviewed By: SIMAMA BUKOBA