TANGOZO

TANGOZO
Latest News
Tuesday, August 2, 2016

JE? LAZIMA BI HARUSI ALIPWE KWA DHAHABU

 Kampeni imezuka nchini Misri dhidi ya desturi ya kuwazawadia mabibi harusi dhahabu chungu nzima wakati wa harusi zao.

Mabwana harusi watarajiwa ambao hawana mali za kuwazawadia wapenzi wao wanasema desturi hiyo ni ghali mno.

Mbali na mahari nyenginezo familia ya bwana harusi hutarajiwa kutoa kile kinachoitwa kwa lugha ya kiarabu "shabka" ambayo ni dhahabu na vito vyenginevyo vyenye thamani na wingi wa vyombo hivyo huonekana kama kipimo cha hadhi ya familia hiyo na vilevile jinsi wanavyomthamini bibi harusi huyo.

Lakini tatizo ni kuwa bei ya dhahabu inazidi kuongezeka kila uchao.

Kwa sasa gramu moja ya dhahabu ya carat 21-ni pauni za Misri 445 sawa na dola $50.

Bwana harusi huyo pia anatarajiwa kununua nyumba mbali na kulipa mahari ya bi harusi.

Sasa kampeni hiyo inayonuiwa kupunguza gharama za ndoa za Misri inazidi kuungwa mkono.

Katika hotuba ya ijumaa kwa wakaazi wa kijiji kimoja katika jimbo liitwalo Qena kazkazini mwa nchi hiyo, wito umetolea maharusi waache kupeana na kupokea zawadi za dhahabu na badala yake watoe zawadi nyenginezo zenye hadhi lakini zisizo ghali.

Ni ujumbe ulioenea kwenye mitandao ya kijamii na tovuti za magazeti kama vile al-Watan.

Wengine kupitia hashtag #Bride's_gift_silver wamependekeza badala ya dhahabu, fedha ndio itumike zaidi kwani bei yake iko chini kidogo.

Waimbaji pia wamejiunga na kampeni hiyo kama vile mwimbaji mashuhuri Amir Teima ambae katika akaunti yake ya facebook anawataka wanandoa ‘mke na mume wafanye kazi kwa bidii na kujenga msingi imara wa familia yao changa badala
ya kutegemea zawadi tu kutoka kwa familia ya mume kwani ‘’harusi si bidhaa wala biashara.’ Amesema.

Viongozi wa kidini kwa upande wao wameunga mkono jambo hilo wakisema litawasaidia wanaotaka kuoa na vilevile kuondoa vishawishi kwa vijana kujiingiza kwenye mapenzi ya nje ya ndoa.

Hata hivyo baadhi ya wanawake wanasema ni utamaduni unaopaswa kudumishwa kwani dhahabu ni sehemu muhimu ya mahari na ni haki bi harusi atuzwe na kuzawadiwa inavyostahili .

  • Blogger Comments
  • Facebook Comments

0 comments:

Post a Comment

Item Reviewed: JE? LAZIMA BI HARUSI ALIPWE KWA DHAHABU Rating: 5 Reviewed By: SIMAMA BUKOBA