Utafiti umebaini kuwa wanawake ambao wametolewa kidole tumbo ama 'appendix' au kutolewa kifindofindo au kifuko ama ''Tonsils'' kwa njia ya upasuaji wanapata uwezo mkubwa zaidi wa kushika mimba.
Utafiti huo wa miaka kumi na tano, uliyofanywa
katika chuo kikuu cha Dundee,ulihusisha uchunguzi wa rekodi za matibabu
ya zaidi ya wanawake nusu milioni wa Uingereza.
Utafitu huu
unawapa akina mama wanatafuta ujauzito afueni kubwa sana na pia
kuwaondolewa wasiwasi kuhusu uoga wa kufanyiwa opereshini ya kuondolewa
kidole tumbo yani appendix kwamba eti itahitalafiana na uwezo wao wa
kupata uja uzito.
Utafiti huu huo pia ilifanyiwa wanawake nusu
milioni waliofanyiwa operesheni ya kuondolewa kifindo findo au tonsils
kwa kiingereza kama kweli inaleta utasa miongoni mwa wanawake.
Mmoja ya watafiti hao Daktari Sami Shimi anasema madakatari wengi walipotoshwa walipokuwa chuoni wakisomea udakatari.
''Chuoni
tulielezwa kuwa kufanyiwa oparesheni ya kuondolewa kidole utumbo yaani
apendix inasababisha utasa na kumfanya mwanamke asiweze kupata
ujauzito''.
Mtafiti huyo ameiambia BBC kuwa oparesheni ya kuondoa kifindo findo au hata kuondoa kidole tumbo ,apendix haisababishi utasa.
Na wamethibitisha hali hii baada ya kuwafanyia utafiti jumla ya wanawake nusu milioni nchini Uingereza.
Daktari
Sami anasema utafiti huu unawahakikikisha wasichana kwamba wakiwa na
matatizo ya 'appendix' au kidole tumbo wasiwe na wasiwasi kwamba
itapunguza uwez\o wao wa kupata uja uzito siku za baadae.
Badala
yake mwanasayansi huyo wa maumbile anasema badala yake kufanyiwa
upasuaji wa kuondoa
sehemu hizo za mwili zikiwa zinauma au kutatiza au
hata zikiwa zinapata maambukizi ya mara kwa mara inamuongezea mwanamke
uwezo wa kujaliwa kupata mimba.
ena kwa haraka sana.
Wanasayansi hawa wanaujumbe maalum tena wa matumaini kwa akina mama.
Nao
wanasema hivi , Pengine tatizo lako la kutoweza kuzaa wewe mama
linasababishwa na matatizo ya kidole tumbo yaani appendix au huenda
unamatatizo ya muda mrefu ya kifindofindo , tonsils, basi harakisha
uende ukafanyiwe upasuaji wa kuondoa Apendix na Tonsils ili uongeze
uwezo wako wa kupata ujauzito na kujaaliwa na watoto.
0 comments:
Post a Comment