Mbunge mmoja nchini Zimbabwe alizua
kizaazaa bungeni pale alitumia chupi za kina mama kusisitiza hatma ya
raia masikini wa nchini hiyo ambao hawana uwezo wa kununua chupi mpya.
Katika
kikao kilichokua kikipeperusha moja kwa moja kwenye runinga ya taifa,
Priscilla Misihairabwi-Mushonga, wa chama cha upinzani cha Movement for
Democratic Change (MDC), alitoa karatasi ya plastiki iliyokuwa na chupi
hiyo. Kisha akamuuliza waziri wa fedha na sera za serikali kuhusiana na
uagizwaji wa chupi kukuu ambayo anasema ni ya bei nafuu na zinasababisha
madhara makubwa kwa afya ya kina mama.
0 comments:
Post a Comment