Bado Yanga wanaendelea kuusaka ushindi wao wa kwanza kwenye hatua ya makundi ya kombe la shirikisho Afrika.
Baada ya kupoteza mechi yao kwanza ugenini dhidi ya MO Bejaia ya
Algeria, leo walikuwa nyumbani wakikipiga dhidi ya TP Mazembe mchezo
uliomalizika kwa Yanga kupoteza tena kwa goli 1-0.
Goli la Mazembe lilitokana na mpira wa adhabu ndogo baada ya Kelvin
Yondani kumuangusha Thomas Ulimwengu nje kidogo ya eneo la hatari. Mpira
wa adhabu ndogo ulimfikia Merveille Bope na kuupachika kambani baada ya
mabeki wa Yanga kushindwa kuuondosha kwenye eneo lao la hatari.
Yanga-mechi 2 bila goli
Tayari Yanga imeshacheza mechi mbili kwenye hatua ya makundi,
wamefungwa zote kwa goli moja (kila mechi) huku wao wakiwa bado
hawajafunga bao hata moja katika mechi walizocheza.
Chirwa, Mahadhi, mambo poa
Nyota hawa wa Yanga walikuwa wanacheza mechi yao kwa mara ya kwanza
wakiwa Yanga huku Mahadhi akicheza mechi ya kwanza ya kimataifa.
Wote kwa pamoja wameonesha uwezo mkubwa kwa muda waliopata nasi ya
kucheza. Mahadhi aliumia na kushindwa kuendelea na mchezo na nafasi yake
kuchukuliwa na Geofrey Mwashiuya huku Obrey Chirwa yeye nafasi yake
ilichukuliwa na Matheo Athony.
0 comments:
Post a Comment