Naibu
Waziri wa Maliasili na Utalii, Eng. Ramo Makani (wa pili kulia)
akikagua eneo la mpaka katika Msitu wa Hifadhi wa Sayaka katika Kijiji
cha Bugatu, Wilayani Magu, Mkoa wa Mwanza hivi karibuni. Anayeongoza
utambuzi wa mpaka huo ni Afisa Misitu na Nyuki TFS Wilaya ya Magu, Ayoub
Mikae (wa tatu kulia). Kulia ni Mbunge wa Jimbo la Magu, Boniventure
Kiswaga. Eng. Makani aliahidi kwa niaba ya Serikali kupitiwa upya maeneo yoye ya Hifadhi yenye migogoro nchini kwa ajili ya kutafutiwa suluhu ya kudumu.
Naibu
Waziri wa Maliasili na Utalii, Eng. Ramo Makani (wa sita kushoto) akiwa
na wajumbe wa Kamati ya Ulinzi na Usalama wa Wilaya ya Magu na baadhi
ya Wananchi wa vijiji vinavyozunguka Hifadhi ya Msitu wa Sayaka
wakikagua mpaka wa hifadhi hiyo hivi karibuni. Kinachoonekana mbele yao
ni Kigingi cha mpaka kinachodaiwa kusogezwa mbele na wananchi wa maeneo
hayo kwa ajili ya kumega eneo la Hifadhi.
Naibu
Waziri wa Maliasili na Utalii, Eng. Ramo Makani (kulia) akizungumza na
wananchi wa vijiji vinavyozunguka Hifadhi ya Msitu wa Sayaka katika
Kijiji cha Bugatu Wilayani Magu Mkoani Mwanza hivi karibuni. Aliahidi kwa niaba ya Serikali kupitiwa upya maeneo yoye ya Hifadhi yenye migogoro nchini na kutafutiwa suluhu ya kudumu.
Naibu
Waziri Maliasili , Eng. Ramo Makani (kulia) akizungumza na wananchi wa
Kijiji cha Bugatu, Wilaya ya Magu, Mkoani Mwanza hivi karibuni wakati
akikagua ramani ya Hifadhi ya Msitu wa Sayaka kubaini maeneo ya mpaka
yenye mgogoro. Eng. Makani aliahidi kwa niaba ya Serikali kupitiwa upya maeneo yoye ya Hifadhi yenye migogoro nchini kwa ajili ya kutafutiwa suluhu ya kudumu.
Mbunge
wa Jimbo la Magu, Boniventure Kiswaga (kulia) akizungumza na wananchi
wa Jimbo lake katika Kijiji cha Bugatu Wilayani Magu hivi karibuni.
Mwananchi
wa Kijiji cha Salama kilichopo kandokando ya Hifadhi ya Msitu wa Sayaka
Wilayani Magu, Charles Kassandiga (kushoto) akitoa ombi kwa niaba ya
wananchi wa kijiji hicho la kupatiwa maeneo ya kulima na kufuga kwa
Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Eng. Ramo Makani (kulia). Eng.
Makani aliahidi kwa niaba ya Serikali kupitiwa upya maeneo yoye ya Hifadhi yenye migogoro nchini na kutafutiwa suluhu ya kudumu.
Naibu
Waziri wa Maliasili na Utalii, Eng. Ramo Makani (kushoto) akiongoza
kikao cha Kamati ya Ulinzi na Usalama cha Wilaya ya Magu alipotembelea
Wilayani humo hivi karibuni kuona eneo la mgogoro katika Hifadhi ya
Msitu wa Sayaka ambapo aliahidi kwa niaba ya Serikali kupitiwa upya maeneo yoye ya Hifadhi yenye migogoro nchini na kutafutiwa suluhu ya kudumu.
0 comments:
Post a Comment