Kiongozi wa Chama Cha ACT Wazalendo, Ndugu Zitto Kabwe ameondoka
Nchini kuelekea Philadelphia Nchini Marekani Kuhudhuria Mkutano Mkuu wa
Chama Cha Democrats (Democratic National Convention) utakaomthibitisha
Bi Hillary Clinton Kuwa Mgombea Urais kupitia Chama hicho.
Wakati Akiwa kwenye Mkutano huo Ndugu Zitto atapata Fursa ya Kufanya
Mazungumzo Na Viongozi mbalimbali wa Kisiasa duniani, Kufanya Kikao Cha
Maandalizi Juu ya Ufunguzi wa Tawi la
Wanachama wa ACT Diaspora la Nchini Marekani pamoja na Kuwa Na
Mazungumzo Maalum na Katibu Mkuu wa CUF, Maalim Seif Shariff Hamad Juu
ya Hali ya Kisiasa ya Zanzibar na Taifa Kwa Ujumla. Zitto na Maalim Seif
ndio wanasiasa pekee nchini walioalikwa kwenye shughuli za chaguzi za
nchini Marekani.
0 comments:
Post a Comment