Serikali inatekeleza agizo la
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Magufuli la
kuhakikisha viwanda vilivyobinafsishwa vinafanya kazi linatekelezwa
tangu mwezi Novemba mwaka 2015.
Hayo yamebanishwa na Waziri wa
Viwanda, Biashara na Uwekezaji Charles Mwijage alipokuwa akijubu swali
la Mbunge wa Manyoni Mhe. Yahaya Massare lililohusu utekelezaji wa ahadi
ya Rais kuvirudisha viwanda vyote vilivyobinafsishwa lakini havifanyi
kazi.
Waziri Mwijage amesema kuwa
Serikali kupuitia Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji inaendelea na
zoezi la kuchambua mikataba ya mauzo kwa viwanda vilivyobinafsishwa
ambavyo ama havifanyi vizuri au vimesimamisha uzalishaji kabisa.
Waziri amebainisha kuwa timu ya
wataalamu toka Wizara ya Viwanda na Ofisi ya Usajili wa Hazina
walifuatilia na kufanya tathimini kwa kutembelea kiwanda baada ya
kiwanda hatua ambayo inasaidia kutafuta ufumbuzi wa matatizo
yaliyopelekea kiwanda kutofanya kazi.
Aidha, Waziri Mwijage amesema
kuwa uchambuzi wa mikataba ya viwanda hivyo unafanyika kwa ushirikiano
na Ofisi ya Msajili wa Hazina pamoja na Wizara za kisekta ikiwemo Wizara
ya Maliasili na Utalii, Wizara ya Nishati na Madini, pamoja na Wizara
ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi.
Hata hivyo, Waziri Mwijage
amesema kuwa katika kutekeleza ahadi hiyo ya Rais, Serikali imetwaa
Kiwanda cha Chai Mponde kilichopo wilaya ya Lushoto mkoani Tanga ambacho
mwekezaji amekiuka makubaliano ya mkataba.
Mbali na hayo, akijibu swali la
Mbunge wa Tabora Mjini Mhe. Emmanuel Mwakasaka lililohusu mpango wa
Serikali kujenga maabara ya kupima ubora na kiwango cha asali
inayozalishwa hapa nchini, Waziri Mwijage amesema kuwa Serikali
inaendelea kuhimiza ujenzi wa viwanda nchini ikiwemo viwanda vya asali
na kuhakikisha vinakuwa na maabara zinazoweza kupima viwango vya msingi.
Waziri Mwijage ameongeza kuwa
kuhusu ujenzi wa maabara mkoani Tabora, Wizara itahakikisha wawekezaji
wanaofuatilia ujenzi wa viwanda vya asali wanakuwa na maabara za kupima
viwango vya msingi vya msingi na kuiachia TBS kuweka viwango vya kitaifa
na kudhibiti viwango hivyo.
0 comments:
Post a Comment