Diambond Platnumz amewataka Watanzania kumpigia kura kwa wingi star
mwenzie wa Bongo Flava Ali Kiba ili tuzo ya MTV EMMA ya Dunia ije
nyumbani.
Diamond amekiambia kipindi cha The Playlist cha Times Fm, Kuwa kama mwaka jana tulibeba tuzo mbili basi tujitahidi kupiga kura kwa wingi ili isionekane Tanzania tumeshuka mwaka huu.
“Kaingia Mwenzangu Ali hivyo tupige kura kwa sababu tukishindwa maana yake Tanzania ndiyo imeshindwa, Justin Bibber alichukua tuzo nne mwaka jana na mie nkafata nikachukua mbili sasa tukiikosa hii tutaonekana tumefeli zaidi” Alisema.
0 comments:
Post a Comment